
Na Beatus
Maganja
WANYAMAPORI
waliopo nchini wana mchango mkubwa katika Sekta ya utalii kwani huchangia zaidi
asilimia 17 katika pato la Taifa.
Akizungumza
katika ndani ya banda la Wizara ya Maliasili na Utalii kwenye maonesho ya
Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni mkoani Dodoma Agosti 4,2024,
Afisa Mhifadhi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA),
Winniefrida Kweka alisema wanyamapori waliopo nchini wana mchango mkubwa katika
pato Taifa, kwani huchangia zaidi ya asilimia 17.
Winniefrida
alitoa kauli hiyo wakati akitoa elimu ya uhifadhi kwa wakazi wa Mkoa wa Dodoma
waliotembelea bustani ya wanyamapori hai iliyopo ndani ya banda la Wizara ya
Maliasili na Utalii kwenye maonesho ya Nanenane mkoani humo.
Alisema wanyamapori
wanachangia sana kwenye sekta ya utalii kwa zaidi ya asilimia 17 za pato la
nchi, asilimia zote hizo huchangiwa na utalii unaohusisha wanyama wa porini.
Winniefrida
alisema kutokana na faida zitokanazo na wanyamapori hao, TAWA inatumia maonesho
ya Nanenane kuwaelimisha watanzania kuachana na mitazamo hasi kuwa, wanyamapori
ni viumbe wasio na mchango chanya kwa Taifa.
Mhifadhi
huyo alisema kutokana na changamoto kutoka kwa baadhi ya wanyamapori wakali na
waharibifu kama mamba, tembo, fisi na wengine, TAWA imekuwa ikielimisha umma
juu ya mbinu rafiki za kuweza kuishi na wanyamapori hao na kuendelea kubaki
salama kwa kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa nao.
Ameweka wazi
kuwa, chanzo kikubwa cha migongano kati ya wanyamapori hasa mamba na binadamu
ni baada ya binadamu anapohitaji mahitaji yake sehemu ambayo wanyamapori hao
wapo kama kwenye majini.
Alisema
kufuatia changamoto hiyo, Serikali kupitia taasisi zake za hifadhi imekuwa
ikitoa elimu ya kujilinda dhidi ya athari zinazoweza kusababishwa na wanyama
hao ikiwa ni pamoja na kusaidia ujenzi wa vizimba vya mfano ili kuepusha
madhara ya wanyamapori hao.
Winniefrida
ametoa wito kwa wavuvi kufanya shughuli zao za uvuvi kwa njia zilizo sahihi na
kuepuka kutega mitego ya samaki sehemu ambazo mamba wapo na kuachana na dhana
iliyojengeka miongoni mwao kuwa, palipo na mamba ndipo samaki wapo wengi.Maonesho ya mwaka huu yaliyobeba kauli mbiu isemayo "Chagua viongozi bora wa Serikali za Mitaa kwa maendeleo endelevu ya Kilimo, mifugo na uvuvi" yalianza Agosti 1, 2024 na yanategemewa kufika kilele Agosti 8, 2024.
No comments