DAWASA waeleza mafanikio na changamoto zao, wamshukuru Dkt.Samia
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mhandisi Mkama Bwire akizungumza katika kikao kazi cha taasisi hiyo, wahariri na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari leo Jumatano Agosti 7,2024 jijini Dar es Salaam
Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya
Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA), limekutana na wahariri na
waandishi wa habari na kueleza mafanikio iliyoyapata katika kipindi cha miaka
mitatu ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu
Hassan.
Amesema
kwasasa uzalishaji wa maji kwa DAWASA umeongezeka kutoka lita milioni 520 kwa
siku hadi lita milioni 534.6 kwa siku, sawa na ongezeko la lita milioni 14.6
kwa siku.
Ameitaja
nyingine ni Changamoto ujenzi wa makazi usiozingatia taratibu za mipango miji,
ushirikiano na wadau (Tanroads, Manispaa) katika kutatua changamoto na uvamizi
katika maeneo ya hifadhi ya miundombinu ya maji.
Kuhusu
miradi mipya, Mhandisi Bwire amesema miradi mipya inayoendelea kutekelezwa ni
pamoja na mradi wa maji Dar es Salaam ya Kusini, uliosainiwa Oktoba 31, 2023,
ambao ni ujenzi wa tanki la ujazo lita milioni 9, wenye thamani ya sh.bilioni
34.5.
Afisa Uhusiano Mwandamizi Ofisi ya Msajili wa Hazina Sabato Kosuri, akizungumza katika kikao kazi kilichowakutanisha wakurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafiri wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA), wahariri na waandishi wa habari leo Jumatano Agosti 7,2024 jijini Dar es Salaam.
Kabla ya
kuanza kwa kikao kazi hicho, Afisa Habari Mwandamizi kutoka Ofisi ya Msajili wa
Hazina, Sabato Kosuri, amewakumbusha wahariri na waandishi wa habari umuhimu wa
vikao kazi hivyo, huku akiwataka kuzingatia yale yote yatakayowasilishwa.
“Ninawaomba
haya yatakayozungumza kwenye kikao kazi hizi yazingatieni, yatawasaidia katika
kazi zenu,” amesema.
Ameongeza
kuwa, DAWASA wanatakiwa kupambana kumaliza kero zilizopo ili kuongeza ufanisi
wa taasisi katika kuwahudumia wananchi, lakini akimtaka kuwaondoa watendaji
ambao hawataki kutekeleza majukumu yao.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mhandisi Mkama Bwire akizungumza katika kikao kazi
Afisa Uhusiano Mwandamizi Ofisi ya Msajili wa Hazina Sabato Kosuri, akizungumza katika kikao kazi kilichowakutanisha wakurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafiri wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA), wahariri na waandishi wa habari leo Jumatano Agosti 7,2024 jijini Dar es Salaam.
Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA), Bi. Everlasting Lyaro akizungumza katika kikao kazi
No comments