Header Ads

ad

Breaking News

RAIS DKT. SAMIA AANZA ZIARA YA KIKAZI RUKWA KWA KUZINDUA HOSPITALI YA WILAYA YA NKASI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akipokea Taarifa kuhusu ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Nkasi kutoka kwa Mhandisi NeophitusNtalwila kabla ya kuizindua tarehe 15 Julai, 2024. Mhe. Rais Dkt. Samia ameanza Ziara yake ya kikazi Mkoani Rukwa ambapo pamoja na mambo mengine atazindua miradi ya maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akimjulia hali mtoto Jumanne Vincent Gustavo anayepatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Nkasi mara baada ya kuzama kwenye mto na kuokolewa. Kushoto ni mama wa Mtoto huyo Getruda Daniel Mambwe Korongwe mkazi wa Namanyere Mkoani Rukwa.  Mhe. Rais Dkt. Samia ameanza Ziara yake ya kikazi Mkoani Rukwa tarehe 15 Julai, 2024 ambapo pamoja na mambo mengine atazindua miradi ya maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo la huduma za dharura katika Hospitali Wilaya ya Nkasi tarehe 15 Julai, 2024. Mhe. Rais Dkt. Samia ameanza Ziara yake ya kikazi Mkoani Rukwa ambapo pamoja na mambo mengine atazindua miradi ya maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Namanyere mara baada ya kuzindua Hospitali ya Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa tarehe 15 Julai, 2024. Mhe. Rais Dkt. Samia ameanza Ziara yake ya kikazi Mkoani Rukwa ambapo pamoja na mambo mengine atazindua miradi ya maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akiwasikiliza Wabunge wa Mkoa wa Rukwa wakati aliposimama kuzungumza na Wananchi wa Namanyere wakati akitoka kuzindua Hospitali ya Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa tarehe 15 Julai, 2024.

Wananchi wa Namanyere Wilayani Nkasi wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati akiwahutubia mara baada ya kuzindua Hospitali ya Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa tarehe 15 Julai, 2024.

No comments