Header Ads

ad

Breaking News

Nargis aifagili chai ya Tanzania

Na Mwandishi Wetu

MISS Tanzania namba tatu mwaka 2003, Nargis Mohamed ametembelea Banda la Chai kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF-2024) na amevutiwa na ladha ya chai inayozalishwa hapa nchini.

Nargis amesema kuwa chai ya Tanzania ina ladha halisi ya chai huku akiwataka wananchi kuiunga mkono kwa kuinunua kwa wingi.

Nargis ambaye pia ni mkulima wa parachichi wilayani Mafinga amesema jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan ya kuwekeza fedha nyingi katika kilimo, zimerahisisha shughuli za kilimo ambapo kwa upande wake ameona faida za jitihada hizo.


No comments