WAHANDISI WAFANYIWA VIPIMO VYA VIASHIRIA MAGONJWA YA MOYO
Wahandisi wakipata huduma katika
banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa Mkutano wa 30 wa
wahandisi washauri Afrika (FIDIC Africa) unaofanyika katika ukumbi wa Kimataifa
wa Mwalimu Nyerere International Convention Center (JNICC), uliopo jijini Dar es
Salaam.
Na Mwandishi Maalumu, Dar es Salaam
TAASISI ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) inatoa huduma za uchunguzi wa magonjwa ya moyo na ushauri wa
lishe bora kwa wahandisi kutoka nchi za Afrika walioudhuria mkutano wa 30 wa
wahandisi washauri Afrika (FIDIC Africa).
Huduma hiyo inatolewa kwa siku mbili katika
viwanja vya ukumbi wa kimataifa wa mwalimu Julius Nyerere International
Convention Center (JNICC) vilivyopo jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia huduma hiyo daktari
kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Samweli George alisema JKCI imeona
umuhimu wa kuwasogezea wahandisi huduma za uchunguzi wa magonjwa ya moyo karibu
kuwapa nafasi ya kuchunguza afya zao.
“Waandisi muda mwingi wanakuwa katika
maeneo yao ya kazi (site) na kukosa nafasi ya kufika Hosptitali kwaajili ya
kuchunguza afya hivyo kupitia mkutano huu tunawapa nafasi ya kupima afya lakini
pia tunawapa elimu ya namna ya kujikinga na magonjwa ya moyo,” alisema Samweli.
Katika kutoa elimu ya mfumo bora wa
maisha Dkt.Samweli aliwataka wahandishi kuwa na tabia ya kuchunguza afya zao
mara kwa mara na kuijua miili yao kwani magonjwa ya moyo wakati mwingine
humtokea mtu bila ya kuonyesha dalili.
Kwa upande wake Mhandisi kutoka
Tanroad, Magdalena Evance aliwashukuru wataalamu wa afya kutoka JKCI kwa
kumfanyia uchunguzi wa afya kwani hajawahi kuchunguza afya yake kama hana
changamoto yoyote ya ugonjwa.
“Leo nimejifunza kitu kikubwa sana
katika maisha yangu, natakiwa kuchunguza afya yangu kila ninapopata nafasi na
nisisubiri hadi niumwe kwasababu tumeambiwa magonjwa yasiyoambukiza wakati
mwingine hayana dalili,” alisema Magdalena
Magdalena alisema baada ya kupima amepata ushauri wa namna ya kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza elimu ambayo ataizingatia kwani kinga ni bora kuliko tiba.
Mtaalamu wa huduma za afya za mtandao
kutoka kampuni ya Cloudscript inayofanya kazi na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) Beatrice Mmari akiwafundisha wahandisi namna ya kutumia huduma ya afya
mtandao kupitia mfumo wa Cloudscript walipotembelea banda la JKCI wakati wa
mkutano wa 30 wa wahandisi washauri Afrika (FIDIC Africa) unaofanyika katika
ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere International Convention Center (JNICC)
uliopo jijini Dar es Salaam.
No comments