Header Ads

ad

Breaking News

Balile aipongeza MSD kufanya kazi na viwanda vya ndani

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile, akitoa neno la shukrani kwa waandaaji wa mkutano, Bohari ya Dawa (MSD)

Na Frank Balile 
MWENYEKITI wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile, amewapongeza Bohari ya Dawa (MSD), kwa jitihada zao za kuhakikisha wanafanya kazi na viwanda vya ndani. 

Ameyasema hayo wakati wa kikao kazi cha maafisa wa MSD na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari kilichofanyika Septemba 27,2023 jijini Dar es Salaam. Balile alisema kuwa, ni jambo zuri sana la kufanya kazi na viwanda vya ndani vinavyozalisha bidhaa za afya, badala ya kuagiza nje ya nchi.

 "Niwapongeza sana kwa uamuzi wenu wa kuvitumia viwanda vya ndani vinavyozalisha bidhaa za afya, inasaidia kupunguza gharama na kuinua uchumi wa nchi," alisema. Balile amesema tangu MSD wafanye mabadiliko, imeonesha muelekeo mzuri sana katika kujali afya za wananchi kwa kuhakikisha dawa na vitendea kazi vinapatikana.

Mwenyekiti huyo wa TEF, amempongeza Msajili wa Hazina, Nehemia Mchechu na timu yake kwa kuanzisha utaratibu wa taasisi zilizo chini yake zinakutana na wahariri na waandishi wa habari kueleza kazi zao. 

"Nampongeza Msajili wa Hazina, ndugu yetu Mchechu kwa kuliona hili, itasaidia sana wananchi kuzifahamu vizuri taasisi na majukumu yake," alisema. 

Alisema kuwa, thamani ya taaluma ya habari inatakiwa kuheshimiwa, ikiwa pamoja na kupata taarifa sahihi kwa wakati sahihi bila vipingamizi. 

Amempongeza Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai, kwa mipango yake mizuri ya kuhakikisha taasisi hiyo inakuwa msaada mkubwa kwa watanzania katika suala la afya.
Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Mavere Tukai (kushoto), akibadilishana mawazo na Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Ofisi ya Msajili wa Hazina, Erick Anthony Mkuti (katikati) na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile katika mkutano wa wahariri na maafisa wa MSD.

Mhariri Joseph Kulangwa atoa ushauri kwa maafisa wa MSD

Kutoka kushoto ni Meneja Uhusiano Bohari ya Dawa (MSD), Eti Kusiluka, Meneja Mipango, Ufuatiliaji na Tathmini, Hassan Ally, Mkurugenzi Mkuu, Mavere Tukai, Mkuu wa Kitengo cha Habafri na Mawasiliano Ofisi ya Msajili wa Hazina, Erick Anthony Mkuti na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, wakishiriki kikao kazi.

No comments