Header Ads

ad

Breaking News

Waziri Aweso amemteua Bi .Nelly Msuya kuwa Kaimu Mkurugenzi Mwauwasa

Bi.Nelly Msuya WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso, amemteua Bi. Nelly Msuya kuwa, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA). Mbali na uteuzi huo, Waziri Aweso ameteua wataalamu kutoka Sekta ya Maji watakaoshughulikia changamoto ya maji kwa wakazi wa Jiji la Mwanzana kusimamia kukamilika kwa mradi wa kuongeza maji katika mfumo wa usambazaji majisafi jijini humo.
Wataalam hao wataongozwa na wataalamu kutoka Wizara ya Maji makao makuu ambao ni Mhandisi Mkama Bwire, Mkurugenzi wa Usambazaji Maji, Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) na Mhandisi Charles Mafie, Mkurugenzi Msaidizi Uendeshaji na Matengenezo, Wizara ya Maji.

No comments