TPB Benki yaipaisha Taswa SC
Ofisa Mawasiliano wa Benki ya TPB, Chichi (kulia) Banda akizungumza jambo mara baada ya kukabidhi mfano wa hundi kwa Mwenyekiti wa Timu ya Waandishi wa mchezo nchini (Taswa SC) Majuto Omary |
Mwandishi
Wetu
Benki
ya TPB imesaidia timu ya Soka na netiboli ya waandishi wa Habari za Michezo
nchini (Taswa Sc) iliyoondoka Jumamosi jijini Dar es Salaam kwenda Arusha kushiriki bonanza
la vyombo vya Habari.
Ofisa
Mawasiliano wa TPB Benki, Chichi Banda amesema kuwa wameisaidia Taswa SC
kutokana na kutambua mchango wao katika kuendeleza michezo kwa vitendo huku
wakiwa ni waandishi wa habari.
Chichi
amesema kuwa wamevutiwa sana Taswa SC ambayo kwa miaka mingi imekuwa ikifanya
vizuri katika mashindano mbalimbalimbali ikiwa pamoja na kuwa mabingwa wa
kihistoria ya bonanza la vyombo vya habari la kanda ya Kaskazini.
“Hii
ni faraja kwetu na tunaomba Taswa SC kuendeleza wimbi la ushindi katika bonanza
hilo, tunaomba muendelee kufanya vyema ili kujiwekea historia zaidi,” amesema
Chichi.
Mwenyekiti
wa Taswa SC, Majuto Omary aliipongeza TPB Benki kwa msaada huo na kuomba wadau
wengine kuunga mkono juhudi za benki hiyo kongwe nchini kuwasaidia waandishi wa
habari.
"Kuna
wadau wengi sana wa waandishi wa habari, tumepeleka maombi kwao, wengine
wametujibu kwa simu tena siku mbili kabla ya kuanza safari kuwa hawana bajeti
na wengine wamekaa kimya kabisa, imetusikitisha sana, tunawashukuru TPB Benki
ambao wamekuwa na sisi kila tunapowahitaji,” amesema Majuto.
Majuto
amesema kuwa waandishi wa habari ni wadau wakubwa katika sekta ya michezo na
wamekuwa mstari wa mbele kuchangia maendeleo ya sekta hiyo, lakini mara kadhaa
wamekuwa wakikumbana na vikwazo vikubwa katika shughuli ambazo zinawahusisha
wao moja kwa moja.
“TPB
Benki ni wadau wakubwa sana kwa Taswa SC, tunawapongeza kwa kujitolea
kufanikisha shughuli hii ambayo sasa kila mchezaji (Mwandishi) ana uhakika wa
kusafiri na kwenda kutetea ubingwa huku Arusha,” alisema Majuto.
Taswa SC imerejea jijini Dar es Salaam Jumatatu ikiwa na imetwaa ubingwa wa soka, netiboli na kukimbiza kuku.
No comments