Tanzania kuwakilishwa na timu mbili katika mashindano ya Cana kanda ya tatu ya kuogelea
![]() |
Mchezaji wa kuogelea wa timu ya Taifa, Sonia Tumiotto akifanya vitu vyake wakati wa mashindano ya Taifa ya kuogelea. |
Mchezaji wa kuogelea wa timu ya
Taifa, Hilal Hemed Hilal akishindana wakati wa mashindano ya Taifa ya kuogelea.
|
Mchezaji wa kuogelea wa timu ya
Taifa, Collins Saliboko akichuana katika mashindano ya Taifa ya kuogelea.
|
Mchezaji wa kuogelea wa timu ya
Taifa, Marin De Villard akionyesha uwezo wake wakati wa mashindano ya kuogelea
ya Afrika Kusini.
|
Mchezaji wa kuogelea wa timu ya
Taifa, Adil Bharmal akifanya vitu vyake wakati wa mashindano ya kuogelea
ya Afrika Kusini.
|
Na Mwandishi wetu
Tanzania itawakilishwa na timu mbili za kuogelea katika michezo ya kanda ya tatu ya kuogelaa ya Afrika yaliyopangwa kuanza Alhamisi katika bwawa la Hopac la jijini.
Tanzania imepewa nafasi ya kuwa na timu mbili kutokana na kuwa
mwenyeji.
Katibu Mkuu wa Chama Cha kuogelea Tanzania (TSA, Ramadhan
Namkoveka amesema timu ya kwanza imepewa jina la Tanzanite ambayo
itakuwa na jumla ya wachezaji 30 na ya pili inajulikana kwa jina la Platinum
ambayo itakuwa na wachezaji 21.
Namkoveka amesema kuwa timu ya Tanzanite itakuwa na wachezaji 15
wanaume na 15 wanawake na ile ya Platinum itakuwa na wachezaji tisa wanawake na
12 wavulana.
Timu hizo zipo kambini Hoteli ya Giraffe chini ya makocha,
Alexander Mwaipasi na Michel Livingstone na zinafanya mazoezi yake kwenye bwawa
la Hopac kila siku.
Wachezaji wanaounda timu ya Tanzanite ni Rania Karume , Chichi Zengeni, Maia Tumiotto, Smriti Gokarn
(Sonia Tumiotto, Anjani Taylor ambao wote wanatoka klabu ya DSC, huku wengine
ni Natalie Abwooli Sanford (MIS), Anna Guild, Emma Imhoff (MSC), Sanne
Kleinveld ( ISM Moshi), Angelica Spence, Tara Behnsen, Tami Triller,Kayla
Gouws na Amani Doggart ambao wanatoka klabu ya Taliss.
Wachezaji wanaume ni Judah Miller,
Elia Imhoff, Delvin Barick, Caleb O'Sullivan, Khaleed Ladha na Matthew Guild
wanatoka klabu ya Mwanza, Chris Fitzpatrick (ISM Moshi), Marin DE Villard
(DSC), Adil Bharmal, Hilal Hilal, Harry McIntosh, Dhashrrad Magesvaran (Taliss)
na wanaotoka klabu ya shule ya kimataifa ya Morogoro ni Joseph
Sumari, Collins Saliboko na Dennis Mhini.
Wachezaji wanaounda klabu ya
Platinum kwa upande wa wanawake ni Shivan Bhatt, Natalia (Taliss),
Charlotte Sanford, Vanessa Dickson (MIS), Rebecca Guild, Meredith Boo
(MSC), Maria Bachmann ( ISM Moshi), Kayla Temba na Maya Somaiya ambao
wote wanatoka klabu ya DSC.
Wanaounda timu ya wanaume ni Aravind
Raghavendran, Mohameduwais Abdullatif (Bluefins), Abraham Kayugwa( ISM Moshi),
Terry Tarimo, Aliasgar Chakera(Taliss), Zeke Boos (MSC), Yuki Omari,
Augustino Lucas (Champion Rise), Fallih Ahmed (Taliss), Carter Helsby (MSC),
Ian Lukaza(ISM) na Emmanuel Stenson wa shule ya kimataifa ya Morogoro.
Namkoveka alisema kuwa
mchezaji Hilal Hilal ambaye yupo kambini Dubai atajiunga na wenzake kesho
katika mashindano hayo yaliyodhaminiwa na Vodacom
Tanzania, Swissair, JCDecaux, Coca Cola, Label Promotions , Print Galore
na Slipway Hotel.
Mbali ya Tanzania, mashindano
hayo pia yatashirikisha waogeleaji kutoka nchi za Uganda, Rwanda, Sudan na
Kenya.
No comments