Header Ads

ad

Breaking News

Sundowns, USM zatinga robo fainali Afrika, Zamalek yatupwa nje ya michuano hiyo



USM Alger ya Algeria na Al Ahly Tripoli ya Libya zimetinga hatua ya robo fainali ya Klabu Bingwa Afrika, huku mshindi wa pili wa michuano hiyo mwaka jana, Zamalek ya Misri ikitupwa nje ya michuano hiyo.


Ushindi wa mabao 4-1 nyumbani dhidi ya Caps United ya Zimbabwe jijini Algiers na kuihakikisha USM kukaa kileleni mwa Kundi B kwa kujikusanyia pointi 11 katika michezo sita iliyocheza.

Ahly Tripoli ilifanikiwa kuwabana mabingwa mara tano wa kombe hilo, Zamalek  kwa kutoshana nguvu kwa mabao 2-2 jijini Cairo na kufanikiwa kufikisha pointi tisa.

Tayari, Esperance ya Tunisia imekamata nafasi ya kwanza Kundi C, baada ya kuilaza Saint George ya Ethiopia mabao 4-0 mjini Tunis.

Mamelodi Sundowns ya South Africa, ambayo pia ilikata tiketi ya kucheza robo fainali, ilitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya V Club ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) mjini Pretoria.

Etoile Sahel ya Tunisia, Ferroviario Beira ya Msumbiji, Wydad Casablanca ya Morocco na bingwa mara nane wa michuano hiyo, Al Ahly ya M isri zimekata tiketi ya kucheza robo fainali.

No comments