Header Ads

ad

Breaking News

Rooney atua rasmi Everton

                                                                 Wayne Rooney
 Mshambuliaji wa Manchester United na mshikilizi wa rekodi ya mabao Wayne Rooney amejiunga na Everton, miaka 13 tangu aihame klabu hiyo.


Rooney mwenye umri wa miaka 31 ameichezea Manchester United mara 559 akifunga mabao 253.

Alitwaa ubingwa wa Ligi Kuu England mara tano tangu aihame Everton kwa pauni milioni 27 mwaka 2004.
"Ninahisi vizuri kurudi, sitangoja kukutana na wenzangu, kuingia mazoezini na kisha kuingia uwanjani kucheza," alisema Rooney.

Rooney anarejea Everton wakati Man United ikikamilisha usajili wa mshambuliaji wa Everton Romelu Lukaku kwa pauni milioni 75.

No comments