Header Ads

ad

Breaking News

Manchester United yaichapa Real Madrid kwa penalti

Andreas Pereira wa Manchestern United (kushoto) na winga wa Real Madrid Gareth Bale, wakati wa mechi ya Kombe la kimataifa iliyopigwa usiku wa kuamkia leo nchini Marekani. (AFP/Getty Image)

 
MIAMBA ya Ligi Kuu England, Manchester United wameifunga Real Madrid kwa mikwaju ya penalti baada ya kumaliza dakika 90 kwa sare ya bao 1-1.

Anthony Martial alitumia juhudi binafsi na kumtengenezea pande Jesse Lingard na kuandika goli la kwanza.

Casemiro aliisawazishia Madrid kwa njia ya penalti baada ya mlinzi mpya wa United Victor Lindelof kumuangusha Theo Hernandez katika eneo la hatari.

Penalti saba kati ya kumi hazikuingia nyavuni.
Haukuwa usiku mzuri kwa Lindelof ambaye aliendeleza makosa yake na kukosa mkwaju wa penalti.

United wameshinda michezo yote minne katika ziara nchini Marekani na watakutana na Barcelona katika fainali siku ya Jumatano.

No comments