TAKUKURU MKOANI PWANI YAZITAJA TAASISI NA IDARA 11 ZINAZOONGOZA KWA MALALAMIKO YA VITENDO VYA RUSHWA
Kamanda
wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa Takukuru Mkoa wa Pwani
Suzan Rymond akiwaonyesha waandishi wa habari ofisini kwake hawapo
pichani orodha ya majina ya taasisi na idara ambazo zimeongoza kwa
malalamiko ya vitendo vya rushwa (Picha na Victor Masangu)
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo wa Takukuru.
NA VICTOR MASANGU, PWANI
TAASISI
ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Mkoani Pwani imezitaja
taasisi na idara zipatazo 11 ambazo zimelalamikiwa kuhusika katika
matukio mbali mbali ya vitendo vya kupokea rushwa kinyume kabisa
na sheria na taratibu za nchi.
Akizungumza
katika mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake wakati akitoa
taarifa ya utendaji kazi wa kipindi cha miezi mitatu kuanzia mwezi
januari hadi machi mwaka huu Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Pwani Suzan
Rymond alisema kuwa wale waliohusika watapeekwa katika vyombo vya
sheria.
Susan
alisema kwamba kwa sasa wamepokea jumla ya malalamiko 49 yanayohusina na
vitendo vya rushwa baada ya kufanya uchunguzi waa wa wameweza kubaini
idara inayoongoza kwa malalaamiko hayo kwa Mkoa mzima wa Pwani ni
serikali za mitaa ambayo ina jumla ya malalamiko 18.
Kamanda
huyo alifafafnua kuwa idara nyingine iliyoshika nafasi ya pili ilikuwa
ni afya ambayo ilipata malalamiko 8,polisi 4,mahakama 3 ardhi 3 sekta
binafsi 3 elimu 2 tanesco 2 fedha 1 vipimo 1 pamoja na maji 1.
“Ndugu
zangu waandishi wa habari leo tumewaita ili kuwapa taarifa ua
utekelezaji wa majukumu yetu kwa kipindi cha kuanzia mwezi januari hadi
kufikia mwezi machi, na katika miezi hiyo tumepata malalamiko mengi
yanayohusina na vitendo vya rushwa katika mkoa wetu wa Pwani.
Aidha
Kamanda huyo alisema malalamiko ambayo wameshayapokea katika ofisi yaa
ni 64 ambapo kati yao 49 ndio yanahusina na malalamiko ya vitendo vya
upokeajiwa rushwa katika idara za serikali pamoja na taasisi mbali
mbali.
Pia
Suzan alisema kwamba kwa sasa katika kuhakikisha wanakomesha vitendo vya
kupokea na kutoa rushwa wataendelea kufanya uchunguzi wa kina katika
maeneo mbali mbali ili pindi watakapowabaini wahusika waweze
kuwachukulia kali na kuwafikisha katika vyombo vya sheria.
Kamanda
huyo alisema hadi sasa tayari kuna jumla ya kesi 22 zinazohusiana na
vitendo vya rushwa ambazo zimeshafikishwa mahakamani,na pia bado kuna
baadhi ya kesi nyingine bado zinafanyiwa uchunguzi zaidi.
Katika
hatua nyingine Kamanda huyu aliwaomba wananchi wote wa Mkoa wa Pwani
kuhakikisha wanatoa taarifa katika vyombo vinavyohusika endapo wakibaini
kuna daily zoozte za mtu kutoa au kupokea rushwa ili sheria iweze
kufuata mkondo wake wa kuwakamata wahusika ambao wamekuwa na tabia kama
hiyo.
No comments