Yondani atoa la moyoni
BEKI wa
Yanga, Kelvin Yondani, ambaye kwa sasa ni majeruhi baada ya kuchezewa rafu
mbaya na Haruna Moshi ‘Boban’ wa Simba, amewaponda wenzake wanaofanya mambo ya
kijinga uwanjani kwa kutafuta sifa kutoka kwa mashabiki.
Yondani
aliumizwa mguu wake wa kulia na Boban, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania
Bara baina ya timu hizo Jumatano iliyopita, hali iliyowafanya wapenzi wa soka
nchini kupatwa na hofu juu ya beki huyo kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu.
Tayari
daktari wa Yanga, Juma Sufiani, aliweka wazi kuwa, Yondani atakuwa nje ya uwanja
kwa takribani wiki mbili.
Kwa kufahamu jinsi baadhi ya
wachezaji wanavyohatarisha maisha ya wenzao kisoka kwa kuwachezea rafu za
kijinga, Yondani amewataka wachezaji kufuata sheria 17 za soka ili kuepuka
kuingia katika migogoro na wenzao, ambayo haina maana.
Akizungumza na SuperStar akiwa
nyumbani kwake Mbagala jijini Dar es Salaam, Yondani alisema kuwa, ni kwa
kufanya hivyo, wachezaji wanaweza kujiepusha kukatiza ndoto za wenzao katika
soka.
“Tuache
kuwasikiliza mashabiki ili tuchezea mpira, kila mmoja amesajiliwa katika timu
yake ili kucheza soka na si vinginevyo,” alisema beki huyo aliyetua Yanga msimu
huu akitokea Simba.
Kauli
hiyo ya Yondani, inakuja huku kukiwa na madai kuwa, Boban alimchezea rafu ile
kwa makusudi ili kuidhoofisha Yanga, katika pambano hilo la watani wa jadi,
madai ambayo hata hivyo, kiungo huyo wa Wekundu wa Msimbazi, ameyapinga, na kusisitiza
kuwa, hakudhamiria kumuumiza ‘rafiki’ yake huyo.
Tayari
Yondani amesema kuwa, amemsamehe Boban kutokana na rafu hiyo aliyomchezea
akiamini ilikuwa ni sehemu ya mchezo.
No comments