Header Ads

ad

Breaking News

TFF yaipiga faini Yanga ya sh. milioni tatu




Kikosi cha Yanga
 
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limeitahadharisha klabu ya Yanga kuvaa jezi zenye nembo ya mdhamini katika mechi zake za Ligi Kuu Tanzania Bara, kwa mujibu wa mkataba kati ya TFF na mdhamni mkuu wa ligi hiyo, kampuni ya simu ya Vodacom.

TFF, imefikia hatua hiyo ya kuitaka Yanga kuvaa jezi hizo, baada ya mabingwa hao wa Afrika Mashariki na Kati kucheza mechi mbili bila kuvaa jezi mpya zenye nembo za mdhamini huyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo,  Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah, alisema kutokana Yanga kukiuka masharti hayo, wameitozwa faii ya sh. milioni 3, kwa mechi hizo mbili, ambapo adhabu hiyo inaweza kuongezeka baada ya kikao cha Kamati ya Ligi kukaa.

“Tunatarajia kuwaandikia Yanga barau ya kuwatoza faini ya sh. milioni 3, kwa kucheza mechi mbili bila ya kuvaa jezi zenye nembo ya mdhamini,” alisema Osiah.

Licha ya mdhamini huyo kutoa vifaa kwa timu zote za ligi kuu, Yanga walishindwa kuzitumia jezi hizo kwa kuwa zina nembo ya mdhamini ina rangi nyekundu na nyeupe, ambazo zinatumiwa na mahasimu wao, Simba.

Kutokana na hilo, Osiah alisema Yanga walilazimika kuwasiliana na mdhamini ili awabadilishie nembo hiyo, lakini juhudi hizo ziligonga mwamba.

“Kikubwa Yanga hawataki kuvaa jezi zenye nembo nyeupe na nyekundu, kwa madai kuwa, hizo rangi zinazotumiwa na mahasimu wao, lakini mdhamini hajakuliana nao, hivyo TFF tumelazimikia kuwasihi wana Jangwani hao,” alisema Osiah.

Osiah alisema lengo la kuwasihi Yanga kuvaa jezi hizo, ni kutaka kuinusuru timu hiyo na adhabu ya kushushwa daraja, kwa mujibu wa kanuni za ligi.

“Moja ya adhabu  ambayo Yanga itawakumba, ni kushushwa daraja kwa mujibu wa kaninu za ligi, ndio maana tunalazimika kuwasihi kabla ya kukumbwa na adhabu hiyo” alisema Osiah.

ciao

No comments