Si Simba, wala Yanga
![]() |
|
KAPSHENI: Mshambuliaji wa Yanga, Jerryson Tegete (kushoto), akiteta
jambo na nahodha wa Simba, Juma Kaseja.
WAKONGWE wa soka hapa nchini timu za Simba na Yanga, zilitoka sare ya bao 1-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mchezo huo
ulikuwa wa kuvutia kwa muda wote, hivyo kutoa bonge la burudani kwa mashabiki
wa soka waliofurika kwenye uwanja huo.
Simba ndio
walikuwa wa kwanza kupachika bao lililofungwa na Amri Kiemba katika dakika ya
tatu ya mchezi huo.
Kiemba alifunga
bao hilo, akiunganisha krosi safi iliyopigwa na kiungo Mwinyi Kazimoto kutoka
wingi ya kulia.
Mabeki wa Yanga
walikosa umakini wa kuuzuia mpira huo, ambao ulikwenda moja kwa moja kwa Kiemba
na kumchambua kipa Yaw Berko aliyechupa kuuokoa bila mafanikio.
Baada ya bao
hilo la mapema, Simba walioneka kutawala mchezo ambapo sehemu ya kiungo
iliyoongozwa na Jonas Mkude na Kiemba, iliweza kuzima moto wa Haruna Niyonzima
na Athumani Iddi ‘Chuji’ wa Yanga.
Kutokana na
Simba kuendelea kutawala safu ya kiungo, timu hiyo iliweza kupanga mashambulizi
yake na kukosa bao dakika ya 12, baada ya shuti la Felix Sunzu kupaa juu ya
lango la Yanga.
Yanga
walionekana kubadilika na kushambulia kwa kushtukiza, ambapo dakika ya 16,
shuti la Stephano Mwasyika lilipita pembeni kidogo ya mwamba na kutoka nje.
Mchezaji kiraka
wa Simba, Shomari Kapombe alishirikiana vizuri na Juma Nyoso katika safu ya
ulinzi, kuwadhibiti washambuliaji wa Yanga, Said Bahanunzi, Hamis Kiiza na
Didier Kavumbagu.
Katika dakika ya
33, shuti la Mbuyi Twite wa Yanga liligonga mwamba waa juu na kutoka nje.
Kwa upande wake,
Kiiza alishindwa kabisa kuonyesha cheche zake na hivyo kutolewa katika dakika
ya 37 na nafasi yake kuchukuliwa na Frank Damayo.
Baada ya
mapumziko, Yanga walianza kwa kufanya mabadiliko ambaapo Nizar Khalfani alitoka
na nafasi yake kuchukuliwa na Kavumbagu.
Kuingia kwa
Kavumbagu kwa upande wa Yanga kulionekana kuipa uhai kwa timu hiyo ambapo
alishirikiana vyema na Bahanunzi katika kulitia mshikemshike lango la Simba.
Kuingia kwa
Kavumbagu, kuliubadilisha mchezo huo ambapo safu ya ulinzi ya Simba ilikuwa na
kazi ya ziada kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara ya Yanga.
Dakika ya 55,
Kavumbagu alitikisa nyavu za Simba, lakini mwamuzi wa kati, Mathew Akrama
alidai kuwa kabla nyota huyo kutoka Burundi kuukwamisha mpira huo nyavuni,
alimchezea vibaya kipa wa Simba, Juma Kaseja.
Yanga waliandika
bao la kusawazisha dakika ya 64 kwa mkwaju wa penalti iliyopigwa na Bahanunzi,
baada ya Nyosso kuunawa mpira uliorushwa na Twite katika eneo la hatari.
Katika kipindi
hicho cha pili, Yanga walionekana kung’ara sehemu ya kiungo jambo ambalo
lilimlazimu kocha wa Simba, Milovan Cirkovic kumtoa Mkude na kumwingiza
Haruna Moshi ‘Boban’, dakika ya 69.
Kutokana na
mchezo huo kutawaliwa na ubabe wa hapa na pale, Simon Msuva alionyeshwa kadi
nyekundu baada ya kumchezea vibaya Nyosso dakika ya 77.
Zikiwa zimesalia
dakika za lala salama, Boban alimchezea vibaya beki wa Yanga, Kelvin Yondani na
hivyo mchezaji huyo kutolewa na kushindwa kuendelea.
Kutokana na rafu
hiyo, Boban alionyeshwa kadi ya njano na mwamuzi Akrama.
No comments