Header Ads

ad

Breaking News

Ngassa kuikosa Coastal Union


Mrisho Ngassa

MABINGWA wa soka nchini, Simba, wameondoka jana kwenda jijini Tanga kuumana na Coastal Union, bila ya kiungo mshambuliaji wake mpya, Mrisho Ngassa.

Ngassa, ataikosa mechi hiyo baada ya kuwa mgonjwa, hivyo atawakosa Wagosi wa Kaya, watakaocheza nao Jumamosi kwenye Uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga.

Akizungumza na gazeti hili jana, Ofisa Habari wa klabu ya Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema kuwa, Ngassa ni miongoni mwa wachezaji wengine sita walioachwa katika msafari wa kwenda Tanga.

Aliwataja wengini walioachwa ni kiungo Kiggi Makassy, Waziri Hamad, Haruna Shamte, Ramadha Chombo ‘Redondo’, na Emmanuel Okwi, aliyekwenda nchini Uganda kuungana na wenzake katika kikosi cha timu ya taifa ‘The Cranes’ 

Kamwaga alisema kwamba, kuhusu Ngassa, ametemwa kwani bado hajapona malaria, ambayo ilimnyima nafasi ya kucheza dhidi JKT Oljoro ya Arusha, mechi iliyopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kuibuka na ushindi wa mabao 4-1.

Ofisa habari huyo alisema kwa upande wa Makassy, aliumia katika mechi ya kirafiki iliyochezwa juzi kwenye dhidi ya Azam FC uliochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex. Simba ilishinda mabao 3-2.

Kamwaga alimtaja mchezaji mwingine anayesumbuliwa na malaria ambaye hakuwemo kwenye msafara huo ni Redondo, wakati Shamte, Waziri na Koman Billi Keita, ni majeruhi.

“Tunakwenda tukiwa na nguvu, na kila mchezaji anaamini kuwa, tutaibuka na ushindi dhidi ya Coastal Union,” alisema Kamwaga.

Kamwaga alisema kuwa, Simba imekamilika kila idara, hivyto kukosekana kwa wachezaji hao, hakutakuwa na pengo lolote, kwani wapo watakaofanya kazi vizuri ya kuwapa raha mashabiki wa timu hiyo. 

Simba, inaongoza Ligi Kuu Bara kwa kushinda mechi tano na kutoka sare moja, ikijikusanyia pointi 16, hivyo wataingia uwanjani kutaka kuendeleza rekodi yao ya ushindi, huku Coastal Union wakiwa chini ya kocha Hemed Morocco, wakitaka kulinda heshima ya nyumbani.


No comments