Header Ads

ad

Breaking News

Makamu wa Rais wa FA Senegal, abwaga manyanga


Louis Lamotte


DAKAR, Senegal
MAKAMU wa Rais wa Shirikisho la Soka la Senegal, Louis Lamotte, amejiuzulu wadhifa wake juzi, baada ya fujo zilizozuka kwenye mechi mjini Dakar na kutolewa kwa nchi hiyo kwenye michuano ya Mataifa ya Afrika mwaka 2013.

“Kama mwanachama wa kamati ya mechi hiyo kati ya Senegal na Ivory Coast, siwezi kuendelea na majukumu kwa kile kilichotokea uwanjani Jumamosi. Hivyo, nafikiri kitu cha kwanza cha kufanya ni kujiuzulu,” alisema Lamotte, akiwaambia waandishi wa habari mjini Dakar.

“Pia, naondoka na kutoa nafasi kwa ajili ya uchunguzi kutokana na fujo zilizotokea.”
Lakini, Rais wa shirikisho hilo, Augustin Senghor, Jumatano iliyopita aliahidi kutojiuzulu kutokana na tukio hilo la vurugu.

Tayari, Ivory Coast wametangazwa rasmi kuwa, washindi wa mechi hiyo, ambayo ilimalizwa, kabla ya muda wake, wakati wageni wakiwa mbele kwa mabao 2-0, yaliyofungwa na Didier Drogba.

No comments