Header Ads

ad

Breaking News

Kagera Sugar yabanwa na JKT Ruvu



 Mwandishi Wetu, Bukoba

Kagera Sugar na JKT Ruvu, leo zimetoka suluhu, katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, iliyopigwa kwenye Uwanja wa  Kaitaba mjini Bukoba, Kagera.

Pamoja na shangwe za kuichapa Yanga kutawala uwanjani hapo, walishindwa kabisa kuzitikisa nyavu za maafande wa JKT Ruvu.

Kwa matokeo hayo, timu hizo zimegawana pointi moja moja, lakini JKT ikinufaika kwa kupanda nafasa moja katika msimamo wa ligi hiyo, hivyo kuwa ya 12, huku Kagera wakiwa na point inane.

Ligi hiyo, itaendelea kesho kwa mchezo mmoja, utakaopigwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza baina ya wenyeji Toto African na Yanga SC.

No comments