Header Ads

ad

Breaking News

Juventus wapata tajiri wa kumsajili Drogba




JUVENTUS, Italia

KLABU ya soka ya Juventus ya Italia, imeanza mikakati ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba.

Tuttosport limesema kuwa, Juve itaweka nguvu zake kumsajili Drogba, ambaye kwa sasa anaichezea klabu ya Shanghai Shenhua ya nchini China. 

Mkurugenzi wa Juve na Kocha Antonio Conte, walikutana baada ya mechi yao dhidi ya Siena na kujadiliana usajili wa mshambuliaji, na kukubaliana kumrejesha mpachika mabao Drogba, barani Ulaya. 

Juve, pia inasaidiwa na mfadhili kuhakikisha mpango huo unakamilika na wanaangalia uwezekano wa kumshawishi mcheka na nyavu huyo kutoka Ivory Coast, kwenda mjini Turin.

No comments