Header Ads

ad

Breaking News

JOKATE AZINDUA CHAPA YA KIDOTI NA KUIBUKA NA KAULI MBIU YA ‘AINISHA UZURI WAKO’

Na Mwandishi Wetu

Miss Tanzania namba mbili mwaka 2006, Jokate Mwegelo, amezindua rasmi lebo yake ya mitindo ya  nywele na nguo ijulikanayo kwa jina la Kidoti Brand.

Jokate ambaye alianza kujihusisha na masuala ya mitindo mwaka jana, alizindua lebo yake hiyo kwenye hotel ya Serena na kuhudhuriwa na wadau mbali mbali wa masuala ya urembo, maonyesho ya mavazi, wanamitindo na wauzaji wa bidhaa hizo kutoka kila kona ya jiji.

Alisema kuwa hatua ya kuamua kuanzisha lebo hiyo ni moja ya mikakati yake ya kujitafutia fedha kama mjasiliamali na lengo lake kubwa ni kutaka kusimama yeye mwenyewe katika maisha bila ya kumtegemea mtu.

Alifafanua kuwa kabla ya kuanzisha lebo na kampuni yake, alifanya utafiti wa hali ya juu, kuhusiana na sekta hiyo na hatimaye kushiriki kwa mara ya kwanza katika maonyesho ya mavazi ya Red Ribbon na sasa kuamua kwenda mbali zaidi kwa kuingia katika fani ya nywele ambazo  anatengeneza yeye mwenyewe.

Amesema kuwa mbali ya kushiriki katika maonyesho mbali mbali, pia atakuwa anasambaza bidhaa zake za nywele na nguo kwenye maduka mbali mbali ili kuwawezesha wananchi kutumia bidhaa zake.

“Lengo langu kubwa ni kutawala soko na kuwa milionea, hiyo ndiyo ndoto yangu pamoja na kuuza bidhaa zangu hasa za nywele kuanzia shs 9,500 na 12,000. Nguo za Kidoti zitatambulishwa rasmi katika soko mwakani (2013) zikifuatiwa na vifuasi vya urembo pamoja na vipodozi,” alisema Jokate.

Alisema kuwa  msingi wa ubunifu wake ni mchanganyiko wa kipekee wa kiini cha utamaduni wa Kiafrika pamoja na mitindo ya kisasa ulimwenguni kwa ajili ya wanawake na wanaume wa kisasa.


 Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kidoti Jokate Mwegelo akizungumza wakati alipozindua rasmi kampuni hiyo inayojishughulisha na Uuzaji wa Nywele za Style mbalimbali  Ubunifu wa mavazi ambapo ameongeza kuwa nywele hizo zimejaribiwa na kukidhi matakwa ya kudumu, kuweza kutumiwa tena na tena, uzito pamoja na msokotano na zitakuwa zikipatikana katika mitindo na urefu mbalimbali zitazotumiwa na wasichana na kinamama. 
Ameongeza kuwa Nywele hizo pia zitawafikia watu wa mikoani pia. Picha zote na dewjiblog.com
Afisa Mkuu Mtendaji wa Kidoti Jokate Mwegelo akitambulisha timu ya watu anaofanya nao kazi katika Kampuni yake kwa waandishi wa habari na wageni waalikwa.
Pichani Juu na Chini ni Models wakionyesha aina tofauti za Nywele za Kidoti zinazotengenezwa na Darling Tanzania.
Selita Style.
Hii ni aina ya Nywele inayoitwa Jokate,
Aina ya Nayomi.
Models katika picha ya pamoja mbele ya wageni waalikwa.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Kidoti Peter Kasiga akielezea ubora wa Nywele hizo na bei zake  kwa wageni waalikwa na wandishi wa habari waliohudhuria uzinduzi huo leo jijini Dar es Salaam.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Kidoti Peter Kasiga pamoja na CEO wa Kidoti Jokate Mwegelo wakijibu maswali kwa waandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo ambapo pia amefafanua kuzinduliwa rasmi kwa tovuti ya kampuni hiyo leo itakayopatikana kupitia anuani ya www.kidotiloving.com
CEO wa Kidoti Jokate Mwegelo katika picha ya pamoja na Models waliovaa nywele za Sanisi za Kidoti.
CEO wa Kidoti Jokate Mwegelo katika picha ya pamoja na timu ya wafanyakazi wa kampuni yake. Kushoto ni Meneja Masoko Bw. Peter Kasiga, Operation Manager wa Faith Lukindo (katikati), Meneja Biashara Bruce Paschal (wa pili kushoto) na Meneja Mauzo Charles Benson.
“Ainisha Urembo Wako” by Jokate Mwegelo.
Pichani Juu na Chini ni Baadhi ya wageni waalikwa na wadau wa tasini ya urembo waliohudhuria uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo katika Hoteli ya Serena.
CEO wa Kidoti Jokate Mwegelo akiwa na mbunifu nguli wa mavazi Khadija Mwanamboka a.k.a Kubwa la maadui.
Jokate Mwegelo akimpiga busu Khadija Mwanamboka kama ishara ya kumushukuru baada ya kuhudhuria uzinduzi wa kampuni yake.
CEO wa Kidoti Jokate Mwegelo katika picha ya pamoja baadhi ya marafiki waliojumuika naye katika uzinduzi wake. Katikati ni Mdau Calvin na Fashionista Bella all the way from UK.
Jokate Mwegelo akishow love na Binamu yake Esi Sebastian na Mdau William Maelecela a.k.a Lemutuz.
Jokate Mwegelo na Cousin Sister wake Esi Sebastian.
CEO wa Kidoti Jokate Mwegelo akiwa na mmoja wa mawakala wake Said Rundika mwenye duka la Jumla Kariakoo mkabala na kituo cha Mafuta cha Big Bon eneo la Msimbazi.
Jokate Mwegelo na rafiki yake kipenzi Bella.

No comments