Header Ads

ad

Breaking News

Chelsea FC yazidi kutakata England




Juan Mata

LONDON, England

MABAO mawili ya kiungo Juan Mata, yamekisaidia kikosi chake cha Chelsea kuibuka na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya mahasimu wao wa London, Tottenham Hotspur, katika mchezo wa Ligi Kuu ya England ,uliochezwa kwenye wa White Hart Lane,  leo.

Chelsea wameendeleza rekodi yao ya kutopoteza mchezo, ambapo bao lao la kwanza liliwekwa nyavuni na beki Gary Cahill.

Tottenham walisawazisha baada ya mapumziko, bao hilo likifungwa na beki William Gallas, kabla ya Jermain Defoe, kufunga bao la kuongoza.

Hilo lilikuwa bao la 200 la Defoe katika kipindi chake cha soka, lakini halikutosha kumpa kocha wa Spurs, Andre Villas Boas

 ushindi, dhidi ya klabu ambayo ilimtimua Machi mwaka huu, baada ya Mata kusawazisha.
Baadaye nyota huyo wa Hispania, alipachika bao lingine na kumwacha kipa wa Spurs, Brad Friedel, akichanganyikiwa.

Kabla ya Tottenham kusawazisha, Daniel Sturridge, aliiongezea Chelsea bao la nne, dakika za nyongeza.

Kikosi hicho cha Roberto Di Matteo, ambao ni mabingwa wa Ulaya, kina pointi 22, baada ya mechi nane.


No comments