Header Ads

ad

Breaking News

Viongozi wa afrika washirikiana na viongozi wa dunia kusukuma ukuaji wa kilimo katika Afrika



(Melinda Gates, Rais Jakaya Kikwete wa Tananzia na Kofi Annan kwenye mkutano wa Mageuzi ya Kilimo cha Afrika mjini Arusha Tanzania)
……………………………………………………………………………………………………………….
Mkutano wa Mageuzi ya Kilimo cha Afrika waanza mjini Arusha Tanzania
“Tuna mwelekeo wa kuweza kupata ufanisi katika juhudi zetu za kuangamiza njaa na umaskini katika Afrika, kupitia njia ya mageuzi ya kilimo.”alisema Rais Kikwete. “Kwa mchanganyiko wa maongozi bora, kuchukuliwa kwa maamuzi sawa na serikali za mataifa yetu ya Afrika, uendelevu wa misaada kutoka kwa wafadhili na kushiriki kikamilifu kwa sekta ya kibinafsi katika nchi zetu na kwingineko kadhalika, mageuzi ya kilimo cha Afrika yanaweza kufikiwa.”
Akifungua mkutano huo, Kofi Annan, Mwenyekiti wa Umoja wa Mageuzi ya Kilimo cha Afrika – Alliance for a Green Revolution in Africa (AGRA) alieleza juu ya ufanisi uliofikiwa tangu mkutano wa kwanza wa AGRF mnamo mwaka wa 2010. Bw. Annan pia alisisitiza juu ya umuhimu wa kuwaboresha wakulima wa mashamba madogo kwa kuwasaidia kwenda mbele kupelekea mazingira ya kilimo cha biashara.
 “Lengo letu la kuongeza uzalishaji na faida kwa wakulima wa mashamba madogo – wengi wao wakiwa ni wanawake – haliwezi kuyumba. Wao ndio wanaotuwekea chakula kwenye meza zetu, Wao ndio wanaotunza rasilamali zetu za ardhi na maji” alisema Bw. Annan. Hatimaye, wao ndio watakao sukuma ukuaji wa uchumi na maendeleo ya Afrika katika karne ya 21.”
 Melinda Gates, Mwenyekiti mshiriki wa Wakfu wa Bill & Melinda Gates, ambaye alikwenda Arusha kuhutubia wajumbe wa mkutano huu, alitambua maendeleo makubwa ya kilimo cha Afrika yaliyofikiwa ndani ya muda wa muongo  mmoja uliopita, na akatoa wito kwa viongozi wa Afrika waendelee kuunga mkono juhudi hizo.
 “Nawahimiza viongozi wa Afrika kuzingatia upya ahadi zenu za kuongeza uzalishaji wa jamii ya wakulima. Nawahimiza kuweka ajenda ya muongo ujao, itakayokuwa na ari kubwa zaidi,” alisema Bi. Gates. “Natumai mtakuwa makini kweli kuhakikisha kwamba ahadi na mipango yenu itapelekea kuwasaidia jamii za wakulima hawa kufikia malengo yao.”

No comments