Header Ads

ad

Breaking News

Thadeo mgeni rasmi pool Taifa



Mchezaji wa pool kutoka klabu ya Meeda ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Paul Daniel,  akicheza dhidi ya mpinzani wake, Mohamed Semtoe wa klabu ya Spida ya Tanga (hayupo pichani), wakati wa mashindano ya Safari Pool Taifa yanayoendelea jijini Mwanza. Katika mchezo huo, Paul Daniel alishinda. Na Mpigapicha wetu.

Na Mwandishi wetu,Mwanza

MKURUGENZI  wa Michezo  wa Wizara ya Habari, Utamaduni , Vijana na Michezo, Leonard Thadeo, kesho anatarajia kuwa mgeni rasmi katika kilele cha fainali za taifa za mashindano ya pool ya Safari Lager (Safari Lager National Pool Championship 2012).

Mashindano hayo yanayodhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) ,kupitia bia yake ya Safari Lager, zitafanyikia kwenye ukumbi wa hoteli ya Monarch iliyopo mkoani Mwanza, ambapo timu za Meeda ya Kinondoni na Kayumba ya Ilala zote kutoka Dar es Salaam, zikiwania ubingwa huo.

Meeda ilifanikiwa kutinga hatua ya fainali baada ya kuichapa Anatory ya Morogoro mabao13-10 katika hatua ya nusu fainali, huku Kayumba ikiichapa 2eyes ya Arusha mabao 13-9, katika mchezo wa nusu fainali.
Kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja (wanaume), Solomon Elias kutoka Mbeya, alikuwa wa kwanza kutinga fainali, baada ya kumfunga Ally Nada wa Manyara mabao 4-0,  hivyo kumsubiri mshindi kati ya Fayuu Stanley wa Arusha na Athuman Seleman wa Morogoro kwa ajili ya kucheza  fainali.

Kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja (wanawake), Cesilia Kileo wa Kilimanjaro na Betty Sanga wa Mbeya, watachuana katika hatua ya fainali, baada ya kushinda michezo yao ya nusu fainali.

Cecilia alimtoa Sada Tulla wa Shinyanga mabao 4-3, wakati Betty alitingahatua hiyo kwa kumfunga Anna Peter wa Iringa mabao 4-0.

Bingwa kwa upande wa timu ataondoka na fedha taslim sh.milioni tano, kombe  na medali za dhahabu, wakati bingwa kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja (wanaume), atajizolea sh.500,000 na bingwa wa mchezaji mmoja mmoja (wanawake), atazawadiwa sh.350,000.

Mbali ya zawadi kwa washindi hao, lakini kuanzia mshindi wa pili kwa upande wa timu hadi wa mwisho, kila moja itaondoka na zawadi za fedha taslim kulingana na nafasi, huku zawadi hizo zikienda pia kwa mchezaji mmoja mmoja wanaume na wanawake.

Mchezaji wa Pool, Mohamed Semtoe wa Klabu ya Spida ya Tanga, akicheza dhidi ya mpinzani wake kutoka Klabu ya Meeda ya Kinondoni jijijini Dar es Salaam, Paul Daniel, (hayupo pichani) wakati wa mashindano ya Safari Pool Taifa yanayoendelea jijini Mwanza. Katika mchezo  huo Mohamed  semtoe  alishindwa.


No comments