TFF YATOA ITC KWA WACHEZAJI WANNE
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC)
kwa wachezaji wanne waliokuwa wakichezea timu mbalimbali nchini.
Wachezaji
hao ni Tony Ndolo aliyejiunga na KCC ya Uganda kutoka Toto Africans, Felix
Amech Stanley aliyekwenda Bahla ya Oman kutoka Coastal Union, Ernest Boakye
kutoka Yanga aliyejiunga na Tripoli Athletics Club ya Lebanon na Derrick
Walulya aliyerejea URA ya Uganda kutoka Simba.
No comments