Header Ads

ad

Breaking News

Simba yaifundisha kazi TFF




Na Mwandishi Wetu
UONGOZI wa klabu Simba, umeitaka Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Soka (TFF), kukutana haraka kujadili suala la mshambuliaji wao, Emmanuel Okwi, aliyepewa kadi nyekundu katika mechi dhidi ya JKT Ruvu.
Mchezaji huyo wa kutegemewa wa klabu hiyo, alikumbana na adhabu hiyo, baada ya kumpiga kiwiko beki wa JKT Ruvu, Kessy Mapande, ambapo Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-0.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Ofisa Habari wa klabu  hiyo, Ezekiel Kamwaga, alisema kwa upande wao wanaitaka kamati ya ligi kukutana haraka, ili kujua hatma ya mchezaji wao.
Lengo la Simba ni kujua mchezaji huyo kama atacheza katika mechi dhidi ya watani wao, Yanga, ambayo inatarajiwa kupigwa Oktaba 3, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Hata hivyo, licha ya Simba kuishinikiza kamati ya ligi kukutana haraka, lakini Kamwaga alikiri kuwa, kanuni zimewabana na hivyo wanataka kujua ripoti ya mwamuzi iliwasilishwa TFF kwa lengo la kamati ya ligi kuijadili.
“Tunafahamu kuwa, kadi nyekundu ya moja kwa moja ni kukosa mechi tatu, lakini inaweza kuwa mbili kulingana na ripoti ya mwamuzi, ambapo katika mechi hiyo, alikuwa Andrew Shamba wa Dar es Salaam,” alisema Kamwaga. 
Kamwaga alisema hofu yao inaweza kuwa ripoti inamtaka Okwi kukosa mechi mbili, lakini kama kamati hiyo ya ligi haitakaa mapema, wanaweza kukosa haki yao ya msingi.
Wakati Simba wakiwa na kigugumiza hicho, TFF hivi karibuni ilizitaka timu za Ligi Kuu kuwa na utaratibu wa kuweka kumbukumbu ya matukio, ili kuepuka migogoro ya mara kwa mara.
Hata hivyo, TFF imedai kuwa, milango ipo wazi kwa klabu ambazo zina mashaka na kumbukumbuku zao, hivyo ni vema kwenda kuhakiki ili kujiridhisha.

No comments