Header Ads

ad

Breaking News

MKALI RICK ROSS “TUFLON DON” KUTOKA NCHINI MAREKANI KUTIKISA SERENGETI FIESTA OKTOBA 6/2012


Mwanamuziki mkali wa Hiphop RICK ROSS TUFLON DON kutoka nchini Marekani ndiye atakayewapa raha mashabiki na wapenzi wa tamasha la Serengeti Fiesta 2012 mara baada ya utangilizi wa matamasha mengine kama hayo kufanyika mikoa mbalimbali hapa nchini imefahamika.
Akizungumza na Mtandao wa Fullshangweblog kwa njia ya simu jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa kamati ya Maandalizi ya Fiesta Bw. Sebastian Maganga amesema mwanamzuki huyo atakuja nchini na kila kitu kiko sawa kwa ajili ya kufanya vitu vyake katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012 hapo Septemba 6 mwaka huu jijini Dar es salaam.
Amewataka mashabiki wa Serengeti Fiesta kuja kumshuhudia gwiji huyo wa muziki kutoka nchini Marekani wakati atakapofanya mambo makubwa jukwaani katika tamasha hilo.
Sebastian Maganga ameongeza kwa jukwaa la Fiesta ni jukwaa ambalo vijana wa kitanzania wanaweza kulitumia vizuri kuonekana kimataifa kutokana na kwamba wanakuwa wanapanda na kufanya kazi jukwaa moja na wanamuziki wa kimataifa kutoka mataifa mbalimbali tangu tulipoanza Shangwe hizi za fiesta zaidi ya miaka 10 iliyopita sasa

No comments