Header Ads

ad

Breaking News

MANENO YA UTANGULIZI YA MENEJA WA BIA YA KILIMANJARO PREMIUM LAGER, GEORGE KAVISHE WAKATI WA MAKABIDHIANO YA MABASI KWA KLABU ZA SIMBA NA YANGA KATIKA VIWANJA VYA OFISI ZA KAMPUNI YA BIA TANZANIA SEPTEMBA 21, 2012







Mkurugenzi Mtendaji wa TBL
Viongozi  wa TFF,
Viongozi wa Klabu za Simba na Yanga,
Wafanyakazi wa TBL,
Mashabiki
Waandishi wa habari,
Wageni waalikwa
Mabibi na mabwana
Habari za asubuhi.
Kazi yangu ni fupi sana kutoa utangulizi na kufafanua zaidi ni kwa nini tuko hapa leo. Hii ni hafla muhimu kwetu sisi wadhamini wa klabu za Simba na Yanga kwani tunatimiza ahadi iliyopo kwenye mkataba na pia tunahakikisha kuwa timu zetu zinapata usafiri wa uhakika na wenye hadhi.

Mabasi haya yote mawili yana thamani ya shilingi milioni 450 na ni muundo wa Yutong.
Ni ya kisasa kabisa kwani yanabeba abiria 51 akiwemo dereva, ni imara kwani chasis yake ni 4x2, injini ya mabasi haya ni aina ya  300 HP Cummins, yana  retarder ya umeme and breki aina ya ABS, yana TV mbili za kisasa, muziki wa nguvu wenye spika nane, milango na mabuti ya kisasa, kioo cha kuangalia nyuma kinachotumia umeme, jokofu na  kiyoyozi.
Tunataka wachezaji wetu wawe na raha wanaposafiri. Hii ndiyo maana tumeamua kutoa mabasi haya ya kisasa.
Pamoja na kwamba TBL inawajibika kununua mabasi hayo kwa mujibu wa mkataba, lakini lengo kuu ni kuona kuwa wachezaji wanakuwa katika mazingira mazuri.
Tunategemea kuwa mtayatunza mabasi haya vizuri na yatatumika kwa manufaa ya klabu hizi.
Nimefahamishwa kuwa mkiondoka hapa mtafanya ziara katika matawi yenu mbalimbali kuwaonyesha mashabiki wenu mabasi haya na hii pia itakuwa fursa nzuri ya mashabiki kukutana na baadhi ya wachezaji ambao hawajawahi kuwaona.
Napenda kusisitiza kuwa baada ya kukabidhi mabasi haya yatakuwa ni mali ya klabu hizi kwa hivyo ni jukumu la kila klabu kutunza vizuri basi lake ili mnaposafiri mujiskie fahari na muendane na hadhi yenu ya klabu bora na zenye mashabiki wengi Tanzania.
Nawatakia kila la heri hasa katika ligi kuu na mashindano mengine ya kimataifa ambayo mtashiriki.
Asanteni kwa kunisikiliza.

No comments