Header Ads

ad

Breaking News

Grupo Raiz yafanya mambo tamasha la Wiki ya Brazil Dar


Hostess


Na  Mwandishi wetu

BENDI ya Grupo Raiz kutoka Sao, Paulo Brazil imefanya onyesho la kufuru la tamasha la Wiki ya Brazil lililomalizika jana Jumamosi kwenye hotel ya Serena.

Grupo Raiz iliweza kupiga nyimbo nyingi maarufu za miondoko ya Brazil kwa mamia wa mashabiki waliofika kujumuika kuadhimisha miaka 190 ya Uhuru wan chi hiyo ambayo inaaminika kuwa ni wafalme wa soka Duniani.

Mashabiki waliofika katika tamasha hilo lililodhaminiwa na hotel ya Serena na Hennessy  kwa kushirikiana na ubalozi wa  nchi hiyo nchini na rais wa mataifa tofauti ambao waliweza kuona baadhi ya tamaduni za nchi yao.

Mashabiki hao walijumuika stejini kucheza pamoja na Balozi wa Brazil nchini, Francisco Luz ambaye alikuwa kivutio kikubwa katika kucheza staili mbali mbali za muziki wa nchi hiyo. Moja ya staili ambayo imewavutia wengi ni Brazilian Twist iliyochanganyika na staili nyingi mbali mbali tofauti.

Mbali ya muziki, waliohudhuria tamasha hilo waliweza kupata vyakula mbali mbali vya asili ya Brazil ambapo viungo vyake vilitoka nchini Msumbiji na kuvutiwa navyo.

 “Tumefuraishwa sana na jinsi mlivyopokea tamasha la wiki ya Brazil ambayo lilianza Jumatatu iliyopita, ni faraja kwetu kuona wote tumesheherehea miaka 190 ya uhuru wan chi hii maarufu duniani,” alisema Alia Hirjee, mkurugenzi wa kampuni ya  QWAY International, ambao ni mawakala pekee wa Moet-Hennessy  afrika Mashariki na waratibu wa tamasha hilo.

Hirjee alisema kuwa waliofika wamefurahia muziki, chakula na kujua baadhi ya tamaduni za Brazil na kuwaoma wawe mabalozi wazuri katika kuutangaza utamaduni huo.


No comments