Header Ads

ad

Breaking News

Coastal yaichapa Kagera Sugar



Na Mwandishi Wetu, Tanga
TIMU ya Coastal Union ya jijini Tanga, jana iliichapa Kagera Sugar mabao 3-2, katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa CCM Mkwakwani, jana.

Katika mchezo huo uliokuwa wa kusisimua, Coastal Union walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 38, lililowekwa kimiani na Daniel Lyanga, baada ya kuunganisha mpira wa konauliopigwa na Said Sued.
Bao hilo liliwaongezea nguvu, ambapo dakika ya 40, Nsa Job aliwainua mashabiki wa Coastal Union kwa kuifungia timu yake bao la pili.

Dakika mbili baadaye, Kagera Sugar walijitutumua na kufanikiwa kupata bao la kwanza kupitia kwa Amandus Nesta.

Nsa aliiongezea timu yake bao la tatu baada ya kumtoka beki wa Kagera Sugar, Salum Kanon na kuukwamisha mpira kimiani.

Hata hivyo, Kagera Sugar hawakukata tama, waliongeza mashambulizi na kufanikiwa kupata bao la pili lililofungwa kwa njia ya penalti, baada ya Sued kumchezea vibaya mshambuliaji mmoja wa wapinzani, ambapo Kanon aliifungia timu hiyo bao hilo.

Katika mchezo huo uliochezwa na mwamuzi Oden Mbaga, ulikuwa wa kuvutia huku mwamuzi huo akichezesha vizuri

No comments