Header Ads

ad

Breaking News

Bahanunzi, Dida, Chuji waitwa Stars


Said Bahanunzi
KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars, Kim Poulsen ametangaza kikosi cha wachezaji 21 kwa ajili ya mechi ya kirafiki itakayochezwa ugenini Agosti 15 mwaka huu.

Akitangaza wachezaji hao jana kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) alisema kuwa, wachezaji hao wanatakiwa kuripoti kambini katika Hoteli ya Tansoma Agosti 8 saa 1 jioni kwa ajili ya kuanza mazoezi siku inayofuata.

Kim alisema kuwa, kikosi hicho cha Taifa Stars kinayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, kitakuwa na Makipa watatu ambao ni Deogratias Munishi (Azam), nahodha Juma Kaseja (Simba) na Mwadini Ali (Azam).

Aliongeza kuwa, Mabeki ni nahodha msaidizi Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Yanga) na Shomari Kapombe (Simba).

Viungo ni Athuman Idd ‘ Chuji’ (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Moshi (Simba), Mrisho Ngassa (Azam), Mwinyi Kazimoto (Simba), Ramadhan Chombo (Azam), Ramadhan Singano (Simba), Salum Abubakar (Azam) na Shabani Nditi wa (Mtibwa Sugar).

Wachezaji wanaounda safu ya ushambuliaji ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe), ya Congo DRC, Said Bahanuzi (Yanga), Simon Msuva (Yanga) na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe), ya Congo DRC.

Kikosi hicho kipya kinatarajiwa kusafiri nje ya nchi kucheza mechi ya kirafiki na timu ambayo haipo ndani ya CECAFA.

No comments