Header Ads

ad

Breaking News

Yanga yatangulia nusu fainali Kagame


Wachezaji wa Yanga wakishangilia baada ya kushinda kwa penalti

*Yapita kwa kuichapa Mafunzo kwa penalti 5-4

MABINGWA watetezi wa michuano ya Kombe la Kagame, Yanga, jana ilikata tiketi ya kucheza hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo baada ya kuiondosha Mafunzo ya Zanzibar kwa mikwaju ya penalti 5-4, katika mechi iliyopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Dar es Salaam.

Katika mchezo huo, Yanga walianza kwa kulisakama lango la wapinzani wao, ambapo dakika ya 23, Hamis Kiiza akiwa tayari ameotea, alizitikisa nyavu za Mafunzo, lakini tayari mwamuzi Thiesy Nkurunziza kutoka Burundi alikuwa amepuliza filimbi yake.

Mafunzo walijibu mashambulizi hayo, ambapo dakika ya 34, Ali Othman Mmanga alliipatia bao timu yake kwa kuunganisha kwa kichwa mpirawa kona uliopigwa na Ally Juma Hassan.

Kipindi cha pili, Yanga walianza mchezo kwa kulisakama lango la Mafunzo, ambapo dakika ya 63, Jerryson Tegete aliyeingia badala ya Rashid Gumbo aliushindwa kutumia vizuri pasi iliyotoka kwa Haruna Niyonzima kwa kupiga shuti kali lililotoka nje ya lango.

Juhudi za Yanga zilizaa matunda dakika ya 46, baada ya Said Bahanuzi kuisaizishia timu yake bao kwa kichwa, huku akiwaacha mabeki wa Mafunzo wakiwa wamesimama bila ya jitihada zozote za kumzuia.

Tegete, jana haikuwa bahati yake kwani dakika ya 81, alipata nafasi nyingine nzuri, lakini alishindwa kufunga baada ya kupiga shuti lililokwenda nje ya lango la wapinzani wao.

Baada ya dakika 90 kumalizika, sheria mikwaju ya penalti ilitumika, ambapo Yanga ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa penalti 5-4, na kuiwezesha timu hiyo inayonolewa na Mbelgiji, Tom Seintfiet kutinga hatua ya nusu fainali.

Katika mechi ya fainali, Yanga watakutana tena na APR ya Rwanda, ambayo iliiondosha kwenye michuano hiyo URA ya Uganda.

Yanga katika hatua ya makundi ilikutana na APR na kufanikiwa kuichapa mabao 2-0, hivyo mechi hiyo inatarajiwa kuwa ngumu.

Penalti za Yanga zilifungwa na Bahanuzi, Hamis Kiiza, Haruna Niyonzima, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Athuman Idd ‘Chuji’, wakati walioifungia Mafunzo ni Salum Said Shebe, , Mohemmed Abdulrahim, Jaku Juma Jaku na Said Mussa Shaban alikosa.

Katika mchezo huo, mchezaji wa Mafunzo, Juma Othman Mmanga alikimbizwa hospitali baada ya kugongana na mchezaji mmoja, madaktari wa timu zote mbili walimtibu, lakini tatizo lake likaonekana kubwa, hivyo kumkimbiza hopsitali kwa ajili ya matibabu zaidi.


Yanga SC:  Yaw Berko/Ally Mustapa ‘Barthez’, Juma Abdul, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Stefano Mwasyika/Idrissa Rashid, Haruna Niyonzima, Said Bahanuzi, Hamisi Kiiza na Rashid Gumbo/ Jerryson Tegete.


Mafunzo:  Khalid Mahadhi Hajji, Ismail Khamis Amour/Yusuf Makame Juma, Said Mussa Shaaban, Salum Said Shebe, Ali Othman Mmanga, Juma Othman Mmanga, Suleiman Kassim ‘Selembe’, Jaku Juma Jaku, Mohamed Abdulrahim, Wahid Ibrahim na Ally Juma Hassan.



Katika mechi ya kwanza, APR ya Rwanda ilifanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali baada ya kuilaza URA ya Uganda mabao 2-1, katika mchezo ulioanza kuchezwa saa nane mchana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mabao ya APR yalifungwa na Claude Iranzi dakika ya tisa na bao la pili lilifungwa dakika ya 34 na Seleman Ndikumana, wakati URA lao lilifungwa na Robert Ssentongo dakika ya 57.
.

Raha ya ushindi, kila mmoja kwa mtindo wake akijiburudisha kucheza.

No comments