Header Ads

ad

Breaking News

Wawili wajishindia bajaji Yanga


  MASHABIKI wawili wa klabu ya soka ya Yanga ya jijini Dar es Salaam, jana walijishidia zawadi za bajaji katika mchezo wa bahati nasibu wa kutuma ujumbe mfupi wa maandishi.

Katika mchezo huo ambao unaendelea, mashabiki 40,000 walituma ujumbe mfupi wa maandishi na wawili kuibuka vinara.

Mshindi aliyejipatia bajaj ni Sinyasi Vicent mkazi wa Masasi mkoani Mtwara mwenye miaka 39, ni karani mkoani hapo.

Sinyasi alipata bajaj hiyo yenye thamani ya sh. milioni 5.5, wakati aliyeondoka na pikipiki ni Amir Jaffar wa Wilaya ya Uyui mkoani Tabora, pikipiki hiyo ina thamani ya sh milioni 1.5.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu, alisema washindi hao walipatikana katika droo iliyochezeshwa jana.

Msimamizi wa shindano hilo kutoka Push Mobile, Talib Rashid, alisema shindano hilo linaendelea na mashabiki wa Yanga wanatakiwa kuendelee kushiriki.

Bahati nasibu hiyo ilisimamiwa na mwakilishi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Bakari Majid.

“Tangu tumeanza zoezi hili, tuna siku 90 na kila siku tumekuwa tukipata mshindi mmoja ambaye hujinyakulia fedha taslimu sh. 50,000, hadi kufikia leo, Yanga wametoa sh. milioni 4.5,” alisema Rashid.

No comments