Header Ads

ad

Breaking News

SHUGHULI ZA KUTAMBULIWA MAITI ZILIZOOKOLEWA KATIKA AJALI YA MELI ZILIENDELEA ZANZIBAR JANA

Baadhi ya Maiti zilizookolewa kutoka katika Meli ya Skagit iliozama hapo jana zikitambuliwa na Ndugu zao na kuruhusiwa Kuzichukuwa kwa ajili ya Kufanya taratibu za mazishi hapo katika Viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar jana.
Baadhi ya Maiti zilizookolewa kutoka katika Meli ya Skagit iliozama hapo jana zikitambuliwa na Ndugu zao na kuruhusiwa Kuzichukuwa kwa ajili ya Kufanya taratibu za mazishi hapo katika Viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar.
 
Balozi wa Marekani Nchini Tanzania Learnhat Alfonso wakatikati akionekana na huzuni Baada ya kuziona Maiti zilizookolewa katika Meli iliozama hapo jana katika Bahari ya Chumbe Zanzibar.Balozi alifika katika Viwanja vya Maisara ili kuona namna shughuli za kushughulikia maiti  zinavyoendelea.
 
Waziri wa Mamboya ndani wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Emanuel Nchimbi alifikakatika Eneo lililohifadhiwa Maiti wa Ajali ya Meli ya Skagit ili kutambuliwa na Ndugu zao na Kupata maelezo kwa Daktari Kiongozi hayupo pichani  Hapo katika Viwanja Vya Maisara Zanzibar.
Baadhi ya Maiti zilizookolewa kutoka katika Meli iliozama na kukosa watu wake zikipelekwa kuzikwa na Serikali katika Eneo la Kama lililotayarishwa makusudi kwa ajili hio.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete mwenye koti nyeusi akiwa na Makamu wapili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Balozi Seif Ali Idi wakihudhuria katika Eneo la Maisara ili kuona namna shughuli za kutambuliwa kwa Mati zilizookolewa katika Meli iliozama ya Skagit zinavyoendelea na kujuwa hatuwa za kuchukuwa.

No comments