Header Ads

ad

Breaking News

Kilimanjaro Lager yaipa Simba sh. mil. 20 kwa ajili ya mkutano mkuu



Na Mwandishi Wetu
MENEJA wa bia ya Kilimanjaro inayozalishwa na Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL), George Kavishe, jana alikabidhi hundi ya sh. milioni 20, kwa ajili ya mkutano mkuu wa klabu ya Simba utakaofanyika Agosti 5, mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kukabidhi hundi hiyo, Kavishe, alisema kuwa, Kilimanjaro Premium Lager inatambua wajibu wake na ina nia ya kweli ya kuendeleza soka nchini.
Alisema kuwa, Kilimanjaro inapenda kuona maendeleo ya klabu ya Simba, ndio maana wameamua kuiunga mkono klabu hiyo ili kufanikisha mkutano mkuu.
Kavishe alisema kuwa, wanaamini mkutano huo utaimarisha ushirikiano kati ya viongozi na wanachama kwa kuwapa nafasi ya kujadili maendeleo ya klabu yao.

“Mtu anapoangalia historia ya klabu hii kongwe ambayo imejengeka kutokana na rekodi nzuri ya mafanikio kwa muda mrefu, utaona ina mamilioni ya wapenzi nchini. Soka ndio mchezo unaopendwa sana, na bia ya Kilimanjaro imekuwa ikitoa mchango mkubwa kusaidia mchezo huu, ambapo leo tunasaidia mkutano mkuu wa Simba ili kusaidia kudumisha uwajibikaji wa klabu kwa wanachama wake,” alisema.
Meneja huyo alisema kuwa, wanatambua wajibu wao kama wadhamini wakuu wa Simba katika kutekeleza mkataba wao, wataendelea kushirikiana kwa kufanya kazi pamoja ili kuhakikisha soka nchini linazidi kukua.
Mkurugenzi wa Uhusiano na Masuala ya Sheria wa Kampuni ya Bia (TBL), Stephen Kilindo (kulia), akimkabidhi Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange (kushoto), hundi ya sh. milioni 20, kwa ajili ya mkutano mkuu wa klabu hiyo utakaofanyika Agosti 5, Agosti mwaka huu. Wanaoshuhudia ni Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe na Katibu wa Simba, Evodius Mtawala. Picha: Executive Solutions.


No comments